Jarida la Mapishi

Keki ya viazi vitamu

Keki ya viazi vitamu | Jarida la Mapishi
  • Maandalizi
    Dakika 50
  • Kupika
    Dakika 40
  • Walaji
    10

Keki ya viazi vitamu, ni keki inayopikwa kwa kutumia viazi vitamu vilivyo sagwa na mdalasini. Keki hii yafaa sana kula katika kipindi cha sikukuu. Keki hii yaweza pia kuliwa wakati wowote. Fuata hatua zifuatazo, ili ujifunze jinsi ya kupika keki hii ya viazi vitamu.

Ingredients

    Directions

    Step1

    Chukua bakuli kubwa. Weka ndani ya hilo bakuli, viazi vitamu, maganda ya chungwa, mafuta ya kupikia, mayai, light brown sugar, pamoja na vanilla extract, kisha changanya vizuri.

    Step2

    Weka mdalasini, chumvi, unga wa ngano, baking powder, pamoja na baking soda, kisha changanya vizuri kwa kutumia, mashine ya kuchanganyia (mixer), hadi utakapo ona mchanganyiko huo umechanganyika vyema na kuwa laini.

    Step3

    Chukua sufuria la kuoka keki (cake pan) lenye ukubwa wa nchi 9, na upake siagi. Chukua bakuli lenye mchanganyiko ulio changanya na mashine ya kuchanganyia, na umimine mchanganyiko huo kwenye sufuria la kuoka keki.

    Step4

    Washa jiko la kuoka, na uweke joto la nyuzi 175° C, kisha acha jiko lipate moto. Jiko likishapata moto, weka sufuria la kuoka keki ndani ya hilo jiko, na uoke kwa muda wa dakika 35 mpaka 40, au hadi utakapo ona keki imeiva na kuwa na rangi ya kahawia.

    Step5

    Keki ikisha iva, iondoe kwenye jiko la kuoka, kisha iweke pembeni ili ipoe, ikiwa bado ndani ya sufuria la kuoka keki. Keki ikishapoa, unaweza kuitoa ndani ya sufuria la kuoka keki, na kuikata kwa ajili ya kula.

    Unaweza Pia Kusoma Hizi

    Leave a Review

    Your email address will not be published. Required fields are marked *


    The reCAPTCHA verification period has expired. Please reload the page.